TUMBATU FM

Breaking News

waandishi wa habari wametakiwa kutoa elimu kupitia vyombo vya habari juu ya athari za mvua

Image result for images waandishi wa habari tanzania
waandishi wa habari wametakiwa kuendelea kutoa elimu katika vyombo vya habari juu ya athari za mvua za masika ili wananchi waweze kujikinga na athari za mvua hizo ambazo zinasababisha hasara kubwa kwajamii.
akifungua mafunzo ya siku moja kwa waandishi wa habari ofini kwake maruhubi juu ya muelekeo wa mvua hizo mkurugenzi mtendaji wa kamisheni ya kukabiliana na maafa zanzibar shaabani seif amesema vyombo vya habari ni sehemu kubwa inayoaminika katika jamii hivyo watakapo endelea kutoa elimu itaweza kupunguza athari za mvua kwa wananchi.
amesema kwa mujibu wa mamlaka ya hali ya hewa mvua za masika zinatarajiwa kunyesha kwa wastani mkubwa hivyo ni vyema kwa vyombo vya habari kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya kujikinga na maafa yanayoweza kujitokeza ikiwemo upotevu wa mali na makaazi yao.

akiwasilisha mada ya muelekeo wa mvua afisa mipango wa kamisheni ya kukabiliana na maafa makame ali simai amesema juhudi za kukabiliana na maafa zinahitaji mashirikiano kwa taasisi mbalimbali hivyo ni vyema kwa wananchi kufuata sheria hususan katika ujenzi ili kuepuka kuziziba njia za kupitisha maji ya mvua.

aidha ametowa wito kwa  serikeli kuimarisha miundombinu ya mitaro iliopo katika makaazi wananchi pamoja na kuwachukulia hatua watu waliojenga nyumba za makaazi katika njia za maji ya mvua ili kuyawezesha maji hayo kutotuama katika nyumba.

No comments