TUMBATU FM

Breaking News

Tumbatu, Uongozi wa CCM unapokea mawazo kwa wanachama wao

Image result for Images CCM MAPINDUZIuongozi wa jumuiya ya vijana wa chama cha mapinduzi ccm jimbo la tumbatu umesema unaendelea kusikiliza mawazo na ushuri kutoka kwa wanachama na viongozi wengine ili kupata mawazo yenye tija ambayo yatapelekea kukikuza chama.

wakizungumza na radio jamii tumbatu mara baada ya kumaliza kikao maalum kilichowahusisha viongozi wa jumuiya hio mwenyekitiwa jumuiya ya vijana jimbo la tumbatu  abdurazak mwadini makame   na katibu wa jumuiya haji sharifu haji wamesema wameamua kufanya hivyo ili kuwashirikisha wanachama wao katika kila hatua inayopitiwa na jumuiya  katika kukuza maendeleo ya chama.

viongozi hao wamesema watajitahidi kuyafanyia kazi mawazo ya wanachama wao ya kuibua miradi ya jumuiya ili kuachana na utegemezi wa viongozi na hivyo kudumaza maendeleo ya chama

kwa upande wake mmoja wa washiriki wa kikao hicho ali moh'd ussi amesema mpango wa kuwahusisha wanachama na  viongozi katika kuibua mawazo ni kuwataka  viongozi kuwa makini katika kuchanganua mawazo ya kila mtu ili mawazo hayo yaweze kutumika kwa wakati muafaka na sio kuchagua na kuaacha ya baadhi ya watu kitendo ambacho kinaweza kukatisha tamaa na kutoa matumaini kwa watoaji wa mawazo hayo.


kikao cha jumuiya ya vijana ya chama cha mapindizi jimbo la tumbatu hufanyika kila mwaka kwa lengo la kutathimini maendeleo ya jumuiya katika kukuza maendeleo ya chama.

No comments